BLOGU HII NI MAALUMU KWA WALE AMBAO WAPO KATIKA MAHUSIANO YA URAFIKI , UCHUMBA , NDOA . JIFUNZE MBINU ZA KUDUMISHA MAHUSIANO YAKO YA URAFIKI , UCHUMBA NA NDOA. PATA MAJIBU KWA NDOA YAKO. " UPENDO HAUNA MWISHO, HAYA NAWAAMURU NINYI KUPENDANA. ENYI WAUME , WAPENDENI WAKE ZENU." (WAKORINTHO 13:8 , YOHANA 15:17 , WAEFESO 5 :25).
Tuesday, 2 May 2017
Thursday, 15 December 2016
Sunday, 11 December 2016
Tuesday, 11 October 2016
MSICHANA WA CHINI YA MIAKA 15 HUOZWA " KILA SEKUNDE SABA"
Save the Children: Msichana wa chini ya miaka 15
huozwa 'kila sekunde saba'
- 11 Oktoba 2016
India ni moja ya nchi ambazo zinaongoza kwa visa vya ndoa za watoto,
ripoti hiyo inasema
Ripoti mpya ya shirika la Save the
Children inasema msichana wa chini ya miaka 15 huozwa kila baada ya sekunde
saba duniani.
Ripoti hiyo inasema watoto wa hadi
chini ya miaka 10 wanashurutishwa kuolewa na wanaume wazee katika nchi kama
vile Afghanistan, Yemen, India na Somalia.
Save the Children wanasema ndoa za
mapema zinaweza kuchangia msururu wa matatizo ambayo huathiri maisha yote ya
msichana.
Mizozo, umaskini na migogoro ya
kibinadamu vinatazamwa kama sababu kuu zinazowaweka wasichana hatarini ya
kuozwa wakiwa bado wana umri mdogo.
"Ndoa za mapema huanzisha
msururu wa matatizo ambayo humnyima msichana haki za kimsingi za kujifunza,
kujikuza na kujivunia maisha yake kama mtoto," amesema afisa mkuu mtendaji
wa Save the Children International Helle Thorning-Schmidt.
"Wasichana wanaoolewa wakiwa
wadogo mara nyingi huwa hawawezi kuendelea na masomo, mara nyingi hudhulumiwa
na waume zao, kupigwa na hata kunyanyaswa kingono. Hupachikwa mimba na pia huwa
hatarini ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa, ukiwemo Ukimwi."
Ripoti hiyo iliyopewa jina Every
Last Girl, imeorodhesha nchi ambazo ni ngumu zaidi kwa wasichana baada ya
kuzingatia elimu, ndoa za watoto, mimba za mapema, vifo vya wanawake
wakijifungua na idadi ya wanawake bungeni.
Chad, Niger, Jamhuri ya Afrika ya
Kati, Mali na Somalia zinashika mkia kwenye orodha hiyo.
Image copyright Getty Images Image
caption Ripoti hiyo inasema wasichana kwenye kambi za wakimbizi wamo hatarini
ya kuozwa wakiwa wadogo
Shirika la Umoja wa Mataifa
linalowashughulikia watoto, Unicef, linakadiria kwamba idadi ya watoto
watakaoozwa wakiwa wadogo itaongezeka kutoka 700 milioni kwa sasa hadi 950
milioni kufikia 2030.
Ripoti hiyo ya Save the Children
imetolewa siku ya maadhimisho ya Siku ya Msichana Duniani.
NDOA ZA UTOTONI JANGA TANZANIA
Ndoa za utotoni janga Tanzania
- 29 Oktoba 2014
Image caption Watoto walioathirika
na ndoa na mimba za utotoni Tanzania
Tanzania ni moja ya nchi zinaoongoza
kwa mimba na ndoa za utotoni, kwa mujibu wa ripoti inayotarajiwa kuzinduliwa
hii leo jijini Dar es Salaam na Shirika la Haki za Binadamu duniani.
Hata hivyo nchi hiyo imepiga
marufuku ndoa hizo, ambapo mtoto wa kike anaruhusiwa kuolewa anapofikisha umri
wa miaka kumi na nane.
Mkoa wa Shinyanga ulio kaskazini
magharibi mwa Tanzania ndio unaotajwa kuongoza kwa mimba na ndoa za utotoni,
ikilinganishwa na mikoa mingine nchini humo.
Takwimu kutoka mashirika mbalimbali
ikiwemo UNICEF zinaonyesha kuwa, kwa siku, watoto 16 wanapachikwa mimba za
utotoni.
Kwa mujibu wa wataalamu, hali hii
imekuwa ikiendelea kwa muda mrefu na kwa asilimia kubwa imezorotesha maendeleo
ya mtoto wa kike katika eneo hilo.
Ili kumwokoa mtoto wa kike kutokana
na janga hili, kumekuwa na jitihada mbalimbali kutoka mashirika yasiyo ya
kiserikali za kuwaokoa hasa wale ambao tayari wameshatumbukia katika dimbwi
hilo.
Shirika lisilo la kiserikali la
Agape limeweza kuwaokoa wanafunzi wa kike wapatao mia mbili, wakiwa wamepitia
ndoa za utotoni. Wengine tayari wamezalishwa wakiwa na umri chini ya miaka 13.
Hivi sasa wanaanza maisha mapya ya kusoma.
Mmoja wa watoto waliokolewa akiwa
amejitambulisha kwa jina la Pili Omar, ana miaka 14 na ni mama wa mtoto mmoja.
na amekubali kueleza kilichomsibu."Niliolewa kwa sababu wazazi wangu
waliniambia sitaendelea kuwa mzigo kwao, hivyo niolewe ili nianzishe mji
wangu."anasema Pili.
Wazazi na walezi wa watoto hawa
wanalaumiwa kwa kuwalazimisha watoto wao kuingia katika ndoa za utotoni. Licha
ya kukithiri kwa ndoa hizo, pia imebainika kwamba asilimia 99 ya ndoa hizo
hazidumu. Harieth Kulwa ni mmoja wa waathirika wa ndoa hizi ambaye ndoa yake
imevunjika."Nilidhai kuolewa ndio kutatatua matatizo yangu, kumbe
nilijiongezea matatizo. Mwanamume aliyenioa kwanza alikuwa mkubwa kwangu, pili
alikuwa mlevi…" Anabainisha Harieth.
Hata hivyo, wanaharakati wa haki za
binadamu wanaulalamikia mfumo mzima wa kusimamia sheria kwa kutowachukulia hatua
kali za kisheria watu wanaobainika kuwasababishia mimba watoto, wakidai kuwa ni
kutokana na vitendo vya rushwa vilivyogubika vyombo vya shERIA.
BBC SWAHILI
BBC SWAHILI
UKATILI WA KIJINSIA BADO NI KIKWAZO NCHINI TANZANIA
Ukatili wa kijinsia bado ni kikwazo nchini Tanzania
- 19 Agosti 2016
Tanzania inakabiliwa na kiwango cha
juu cha ukatili wa kijinsia ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, pamoja na vipigo
kwa wanawake kutoka kwa waume zao licha ya juhudi mbali mbali za kupinga hatua
hiyo na sheria kali kutungwa bado matukio ya aina hii yanazidi kuongezeka.
Utafiti wa hali ya afya ya
uzazi,mtoto na malaria wa mwaka 2015/2016 unaonesha kuwa idadi ya wasichana
wanaopata watoto katika umri wa miaka 15-19 imeongezeka mpaka kufikia asilimia
27 mwaka 2015 kutoka asilimia 23 mwaka 2010.
Kwa muujibu wa utafiti uliofanywa na
UNICEF wa mwaka 2015,Tanzania ina asilimia 3.5 ya watoto wa umri wa miaka 7-17
walio nje ya shule.
Hii inajumuisha watoto takriban
milioni 2 walitakiwa kuwa shule za msingi na watoto takriban milioni 1.5
waliotakiwa kuwa shule za sekondari.
Aidha utafiti huo umetanabahisha
kuwa katika kila watoto watano wa umri wa kuwa shule ya msingi,kuna mtoto
ambaye hayuko shuleni na katika kila watoto watano wa umri wa kuwa shule ya
sekondari kuna watoto zaidi ya wawili ambao hawako shuleni kutokana na sababu
mbali mbali.
Katika harakati za kutokomeza ndoa za utotoni ,ukatili
wa kijinsia kwa mtoto wa kike na wanawake licha ya kuwapa mafunzo maafisa
maendeleo ya jamii ,maafisa ustawi wa jamii na hata polisi na kuwajengea uwezo
wasichana ,vilabu 350 vya wasicha vimeundwa nchini Tanzania ambao wanatambua
haki zao za msingi.
BBC SWAHILI
Subscribe to:
Posts (Atom)