Tuesday 11 October 2016

UKATILI WA KIJINSIA BADO NI KIKWAZO NCHINI TANZANIA



Ukatili wa kijinsia bado ni kikwazo nchini Tanzania
  • 19 Agosti 2016

Tanzania inakabiliwa na kiwango cha juu cha ukatili wa kijinsia ikiwemo ndoa na mimba za utotoni, pamoja na vipigo kwa wanawake kutoka kwa waume zao licha ya juhudi mbali mbali za kupinga hatua hiyo na sheria kali kutungwa bado matukio ya aina hii yanazidi kuongezeka.


Utafiti wa hali ya afya ya uzazi,mtoto na malaria wa mwaka 2015/2016 unaonesha kuwa idadi ya wasichana wanaopata watoto katika umri wa miaka 15-19 imeongezeka mpaka kufikia asilimia 27 mwaka 2015 kutoka asilimia 23 mwaka 2010.


Kwa muujibu wa utafiti uliofanywa na UNICEF wa mwaka 2015,Tanzania ina asilimia 3.5 ya watoto wa umri wa miaka 7-17 walio nje ya shule.

Hii inajumuisha watoto takriban milioni 2 walitakiwa kuwa shule za msingi na watoto takriban milioni 1.5 waliotakiwa kuwa shule za sekondari.


Aidha utafiti huo umetanabahisha kuwa katika kila watoto watano wa umri wa kuwa shule ya msingi,kuna mtoto ambaye hayuko shuleni na katika kila watoto watano wa umri wa kuwa shule ya sekondari kuna watoto zaidi ya wawili ambao hawako shuleni kutokana na sababu mbali mbali.


Katika  harakati  za   kutokomeza   ndoa  za  utotoni ,ukatili wa kijinsia kwa mtoto wa kike na wanawake licha ya kuwapa mafunzo maafisa maendeleo ya jamii ,maafisa ustawi wa jamii na hata polisi na kuwajengea uwezo wasichana ,vilabu 350 vya wasicha vimeundwa nchini Tanzania ambao wanatambua haki zao za msingi.

 BBC  SWAHILI

No comments:

Post a Comment