‘’Ninatamani
mke/mume wangu angekuwa kama fulani, ninatamani ndoa yetu ingekuwa kama
kina fulani , kama tungekuwa na kitu x kama kina fulani tungekuwa … ni
baadhi ya maneno ya wanandoa ambao hawajui kuwa maneno kama hayo huwa ni
sumu kwenye mahusiano yao.
Katika mahusiano ya ndoa, kama
wanandoa wakishaanza kulinganishana na wengine, yaani kila mmoja
anatamani mwenza wake angekuwa kama fulani hapo ndiyo mahali unapoanza
kupoteza upekee wa mwenza wako.
Njia rahisi ya kupoteza upekee wa
mwenza wako ni kumlinganisha na mwingine. Natamani ungekuwa kama
fulani, ni maneno ambayo yanapoteza nguvu sana na kufanya wanandoa kuwa
dhaifu. Kamwe usimlinganishe mwenza wako na mtu mwingine.
KAVA IJUE NJAA YA WANANDOA
Tambua
kuwa kila mtu ana upekee wake, na ukianza kulinganisha mwenza wako na
mtu mwingine ni kumfedhehesha kama siyo kumkosea heshima.
Unapomlinganisha mwenza na mtu mwingine ni rahisi kumpotezea nguvu ya
kujiamini.
Na kama unavyojua binadamu ni viumbe wa hisia,
unapomlinganisha anajihisi kutothaminiwa na hitaji la kila mwanadamu ni
kuhisi anathaminiwa.
Ni rahisi kupoteza ladha ya mahusiano yenu
pale unapoanza kumfananisha mwenza wako na mtu mwingine. Kama vile
chakula kilichokosa chumvi kinakuwa hakina ladha ndivyo ilivyo kwa
mahusiano yetu pale tunapokuwa tunataka wenza wetu wawe kama kina fulani
tunakuwa tunapoteza tena ile ladha au upekee wao juu yetu.
Huwezi
kumpata mtu aliyekamilika kwenye kila eneo la maisha yako, hata wale
ambao unawatamani wawe kama mwenza wako nao wana mapungufu mengi tu
kushinda hata ya huyo mwenza wako.
Inabidi ifikie mahali urudi
kwenye lengo lako kuu la ndoa au mahusiano yenu, kuna kitu ambacho
kilikuvuta kwa mara ya kwanza mpaka ukawa na huyo ambaye unaye leo hii
hivyo basi siku zote angalia hilo.
Jiulize ilikuwaje au nini
kilichokufanya uwe na mwenza uliye naye sasa? Ukiwa ni mtu wa kujihoji
utakua na maana kwenye maisha yako ya ndoa lakini mtu ambaye hajioji
hana sababu ni mtu ambaye tayari amepoteza maana ya maisha ya ndoa.
Lazima uwe na sababu kwenye kila kitu, kwanini unafanya hicho
unachofanya sasa unapokuwa na sababu basi unakuwa na maana lakini
ukikosa sababu unapoteza maana.
Hatua ya kuchukua leo;
usimlinganishe mwenza wako na mtu mwingine yeyote yule. Kumbuka mwenza
wako ni wa pekee sana hawezi kuwa kama wengine na unapomlinganisha jua
unauwa upekee wake.
Siku zote angalia sababu iliyokufanya uwe na
huyo ambaye unaye leo. Usitamani ya watu bali mtengeneze mwenza wako awe
vile unavyotaka awe na kwa upendo na umoja mtaliweza hilo.
Hivyo
basi, wakati mwingine tunatakiwa kuchukuliana kwenye maisha ya ndoa,
tuwavumilie wenzetu kadiri ya madhaifu yao, tuangalie mazuri yao na
kuyatumia vema , lakini tukiweka fokasi yetu kwenye mabaya tutazidi
kuona mabaya yao kila siku na mwisho wa siku mtachokana haraka.
Maisha
ya ndoa ni maisha mafupi sana hivyo ni vema mkapendana kwa muda kwani
wengi mnakutana tayari mmeshakuwa watu wazima na mkiishi mtaishi kwa
muda tu kumalizia safari ya maisha yenu hapa duniani.
BLOGU HII NI MAALUMU KWA WALE AMBAO WAPO KATIKA MAHUSIANO YA URAFIKI , UCHUMBA , NDOA . JIFUNZE MBINU ZA KUDUMISHA MAHUSIANO YAKO YA URAFIKI , UCHUMBA NA NDOA. PATA MAJIBU KWA NDOA YAKO. " UPENDO HAUNA MWISHO, HAYA NAWAAMURU NINYI KUPENDANA. ENYI WAUME , WAPENDENI WAKE ZENU." (WAKORINTHO 13:8 , YOHANA 15:17 , WAEFESO 5 :25).
Showing posts with label KUJENGA FAMILIA NA MAHUSIANO. Show all posts
Showing posts with label KUJENGA FAMILIA NA MAHUSIANO. Show all posts
Thursday, 19 December 2019
Tuesday, 2 May 2017
Thursday, 15 December 2016
Thursday, 9 June 2016
KWANINI NDOA ZA SASA HAZIDUMU ?
Brigedia Generali mstaafu Francis Mbena,mwenye umri a miaka 86 alifunga ndoa akiwa na miaka 25 ,mwaka 1965
Imezoeleka kwamba ndoa za kikatoliki
zikifungwa zimefungwa
pamoja na sharti hilo ,viwango vya ndoa zinazovunjika
zinaendelea kuongezeka na kufuatia hali hiyo,kanisa katoliki limeamua kuanzisha
tuzo maalumu kwa wandoa wakongwe zaidi kwa mwaka huu katika kanisa hilo.
Kanisa Katoliki jimbo kuu la Dar es
salaam wameandaa kliniki ya ndoa ili kuweza kuwapa fursa wanandoa kuimarisha
ndoa zao kiimani,Padre Novatus Mbaula ambaye ni mkurugenzi wa ndoa na familia
anaeleza lengo la kliniki hii ni kuwapa nafasi wanandoa wa katika makundi
mbalimbali kukaa pamoja kupata neno la Mungu na kuweza kuongea juu changamoto
zao mbalimbali kuongea kuhusu maisha yao ya ndoa.
Ni nafasi ambayo wanandoa ambao wana
uzoefu mkubwa katika ndoa wanaweza kuwafaidisha wanandoa wachanga lakini pia
changamoto katika ulimwengu wetu wa sasa changamoto bado ni zilezile.
Pesa
zimeharibu ndoa nyingi
Miongoni mwa watu waliohudhuria
kliniki hii ni wanandoa wenye ndoa yenye miaka 61,brigedia Generali mstaafu
Francis Mbena,mwenye umri a miaka 86 alifunga ndoa akiwa na miaka 25 ,mwaka
1965 Juni,anasema wao zamani walikua wanafuata mtu na familia gani na ina vigezo
gani?
Walikua wanaangalia tabia kama
msichana hana tabia nzuri huoi huko; kama familia ina watu walevi uwaendei na
unatafuta familia yenye watoto wenye tabia nzuri ili na wewe uweze kupata
watoto wenye tabia nzuri.
Wakati mke wake ambaye ni Maura
Stephen Mbena ambaye anasema asili yake ni Nyoni,yeye anasema ukiweza
kumvumilia mwezako na ukamsamehe basi unaishi tu maana kukwaruzana kupo
hakuishi na kikubwa ni kuvumilia.
Na katika mila na desturi za kabila
yake ya wangoni, msichana kabla hajaolewa anaanapewa maneno na wazee ambao
wazazi wako wamewaamini wanakupa msafara wote wa maisha ya ndoa,kwamba
unapokwenda kuna matatizo pengine wakwe zao hawatakupenda au hautafanya vizuri
kule na wanakupa muelekeo wa maisha ukavumilie na ukafanye hivi hivi lakini
kikubwa sana ni sala.
Ndoa ni maisha yenye tafsiri
nyingi,Bwana na bi.Alphonce Hurick walioko kwenye kipindi cha mwaka mmoja wa
ndoa,wao wanaona maisha ya ndoa ni maisha yenye furaha,amani na upendo na ni
maisha tofauti kabisa wakati kila mmoja akiishi peke yake peke yake,kwani hata
kama una msongo wa mawazo kama ndoa yako ina furaha basi hayo matatizo yanakuwa
hayapo kama ndoa yako ina upendo.
Bi.Kigadie ambaye yuko kwenye ndoa
kwa miaka 46 na miezi mitano anaeleza jinsi walivyoingia kwenye ndoa na jinsi
vijana wanavyoingia kwenye ndoa katika miaka ya sasa.
Anasema wengi hawakupata mafunzo ya
kujua uchumba ni nini maana mapema mno wanageuza uchumba kuwa mme na mke kabla
hawajapata sakramenti ya ndoa,sasa hilo ni tatizo ambalo wanajikuta wamepata
ujauzito sasa ndoa inakuwa ya shuruti unaweza kuwa hata bwana alikuwa hana nia
ya ndoa zaidi ya tamaa za kimwili na kimaisha.
CHANZO CHA TAARIFA: BBC SWAHILI, 09/06/2016
Subscribe to:
Posts (Atom)